Psalms 132:1-5

Maskani Ya Mungu Ya Milele Katika Sayuni

(Wimbo Wa Kwenda Juu)


1 Ee Bwana, mkumbuke Daudi
na taabu zote alizozistahimili.


2 aAliapa kiapo kwa Bwana
na akaweka nadhiri kwa Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo:

3 b“Sitaingia nyumbani mwangu
au kwenda kitandani mwangu:

4 csitaruhusu usingizi katika macho yangu,
wala kope zangu kusinzia,

5 dmpaka nitakapompatia Bwana mahali,
makao kwa ajili ya Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo.”

Copyright information for SwhKC